Fatuma akiwa na watoto wake baada ya kupatiwa fedha na kununua mahitaji ya watoto.
KUFUATIA mtandao wetu kuandika habari iliyokuwa inasema “Watoto njiti mapacha watelekezwa na baba yao’’, hatimaye Wasamaria wema wajitokeza kumsaidia mama wa watoto hao, Fatuma, ambaye amezaa mapacha Rahma na Rahmu.
Watoto wakiwa wamelala pembeni ya makopo ya maziwa yaliyotokana na msaada huo.Akizungumza na mwandishi wetu leo alisema: ‘’Naishukuru sana kwa kuyatangaza matatizo yangu pia namshukuru sana dada Mary Chibwana kwa kujitolea kunipatia fedha kwa ajili ya mahitaji ya watoto. Vilevile nawashukuru wote walionisaidia kwa fedha, salamu na hata ushauri.”
Makopo ya maziwa ya watoto yaliyonunuliwa.PICHA NA GPL