Ndugu wasomaji wetu tunaomba support yenu kwa kutangaza nasi hapa kwenye hii blog kwa bei nafuu ili tuweze kuendelea kutoa habari bila tatizo lolote. Wasiliana nasi kupitia namba +255713363965 / +255755274953. Tunashukuru kwa ushirikiano wenu.
Waziri wa Mawasiliano, Sayansi na Teknolojia Mhe. Prof. Makame Mbarawa (Mb), kwa mamlaka aliyonayo chini ya Sheria Na. 12 ya mwaka 2003 ya Mamlaka ya Udhibiti wa Mawasiliano Tanzania Kifungu cha 13 (1) amemteua Dkt. Ally Yahaya Simba kuwa Mkurugenzi Mkuu wa Mamlaka ya Mawasiliano Tanzania (TCRA) kwa kipindi cha miaka mitano kuanzia tarehe 6 Julai 2015.
Kabla ya uteuzi huo, Dkt. Ally Yahaya Simba alikuwa Mkurugenzi wa Idara ya Teknolojia ya Habari na Mawasiliano wa Wizara ya Mawasiliano, Sayansi na Teknolojia.
Imetolewa na:
Selina Lyimo
KAIMU KATIBU MKUU
Wizara ya Mawasiliano, Sayansi na Teknolojia