Ndugu wasomaji wetu tunaomba support yenu kwa kutangaza nasi hapa kwenye hii blog kwa bei nafuu ili tuweze kuendelea kutoa habari bila tatizo lolote. Wasiliana nasi kupitia namba +255713363965 / +255755274953. Tunashukuru kwa ushirikiano wenu.

Katibu wa NEC, Itikadi na Uenezi Nape Nnauye akisisitiza jambo wakati akizungumza na uongozi wa New Habari Corporation Ltd, hasa kuhusu masuala ya wagombea Urais

Mhariri Mtendaji wa New Habari Corporation, Absalom Kibanda akimkaribisha Nape

Mhariri Mtendaji wa New Habari Corporation Absalom Kibanda, akitambulisha kwa Nape uongozi wa magazeti ya kampuni hiyo.
NA BASHIR NKOROMO
Chama Cha Mapinduzi (CCM) kimesema, hakuna kitakayempitisha kugombea urais 2015, kwa presha za makundi au wapambe.
Akizungumza kwa nyakati tofauti katika vyumba vya habari vya magazeti ya Habari Corporation, na Mwananchi Communication Ltd, jijini Dar es Salaam, leo, Katibu wa NEC, Itikadi na Uenezi, Nape Nnauye amesema, mfumo wa CCM katika kuwapata wagombea ni imara kiasi kwamba hautaweza kuathiriwa na presha za makundi wakati wa kuteua mgombea urais katika uchaguzi mkuu mwaka huu.
Amesema, ni vigezo vinavyozingatia kanuni na katiba ya Chama tu ndivyo vitakavyomuwezesha anayetaka kupeperusha bendera ya CCM kupitishwa na Chama, vinginevyo haitawezekana hata kama ana makundi yenye presha kiasi gani.
"Chama hiki kina mfumo na taratibu ambazo haziwezi kusukumwa na presha za wapambe wa mgombea yeyote, na hata kumbukumbu zinaonyesha kwamba katika chaguzi zilizopita, wamewahi kuwepo wagombea wenye makundi yenye presha kiasi cha kudhaniwa ndio wangeteuliwa, lakini baada ya kufika mbele ya taratibu na kanuni waliachwa na nafasi kupewa wengine", alisema Nape.
Alisema, kanuni na taratibu ndizo mwamuzi wa mwisho katika kuteua wagombea wa CCM, "Sisi tukisema wanaotaka nafasi hii njooni mjipime hapa, mmojawapo akijaiona hatoshi lakini kwa ujanja akaongeza matofali kupata urefu... huyo taratibu zitatumia kuondoa matofali ili abaki kama alivyo kuona kama anatosha", alisema Nape.
"Na katika utaratibu huu wa kuondoa matofali ndiyo watajitokeza baadhi yao kulalamika kwa sababu itauma kidogo", alisema.

Katibu wa NEC, Itikadi na Uenezi, Nape Nnauye akiingia katika ofisi za Kampuni ya Habari Corporation Ltd, kendelea na ziara katika vyombo vya habari aliyoianza wiki iliyopita. Kushoto ni Mkurugenzi wa Mawasiliano ya Umma wa CCM, Godfrey Chongolo

Nape akisalimiana na Mhariri Mkuu wa Habari Corporation Denis Msaky baada ya kuingia chumba cha habari

Nape akisalimiana na Matinyi ambaye ni mmoja wa wahariri katika kampuni hiyo ya Habari Corporation, wachapishaji wa magazeti ya Mtanzania, Rai na Dimba

Napa kisalimiana na Mhariri wa Msanifu wa Habari wa Mtanzania Hamis Mkotya

Nape akiwa katika chumba cha habari cha Mtanzania

Nape akitazama picha iliyomvutia katika chumba cha habari cha Mtanzania, ambayo alionyeshwa na Msaky.

Picha yenyewe ni ya Rais wa sasa Jakaya Kikwete, Rais Mstaafu Benjamin Mkapa, Waziri Mkuu wa zamani Edward Lowassa na Muasisi wa Habari Corporation, Jenerali Ulimwengu

Nape akionyeshwa chumba cha habari cha chenye mkusanyiko wa madawati mbalimbali ya magazeti ya Mtanzania Rai na Dimba

Nape akisalimiana na Mhariri wa habari za Siasa Sarah Mosi

Nape akisalimiana na Mhariri wa habari wa Mtanzania, Bakari Kimwanga

Nape akisalimiana na John Mlinda

Nape akisalimiana na Mkuu wa Kitengo cha Usanifu

Nape akiwa katika picha ya pamoja na wasanifu wa kurasa

Nape akizungumza zaidi

Nape akizungumza mambo ya Mkurugenzi Mtendaji wa Habari Corporation, Hussein Bashe baada ya mazungumzo ya ndani

Wakuu wa New Habari Corporation wakiagana na Nape nje ya ofisi za kampuni hiyo

Katibu wa NEC, Itikadi na Uenezi Nape Nnauye akikaribishwa na Mhariri Mkuu wa Mwananchi, Bakari Machumu baada ya kuwasili kwenye ofisi za Kampuni ya Mwananchi Communications Ltd leo

Bakari Machumu akimkaribisha Nape ofisini kwake. Kushoto ni Chongolo

Nape na Machumu akiwa katika chumba cha habari cha magazeti ya Mwananchi na The Chitizen

Nape akizindikizwa na Machumu wakati wakienda ukumbini kwa ajili ya mazungumzo zaidi

Nap0e akizungumza na uongozi wa magazti ya kampuni ya Mwananchi Communications Ltd

Nape akisisitiza jambo wakati akizungumza na uongozi wa magazeti ya kampuni ya Mwananchi Communications Ltd

Nape akimpatia zawadi ya kalenda ya CCM, Bakari Machumu, mwishoni mwa mazungumzo

Haya kwaherini mbaki salama...

"Mimi pia nipo hapa" Angetile Oseah akimwambia Nape baada ya kukutana wakati akiondoka ofdisi za Mwananchi Communication Ltd.

Nape akiagana na Bakari Machumu mwishoni mwa mazungumzo. Picha na Bashir Nkoromo