Quantcast
Channel: PAMOJA BLOG
Viewing all articles
Browse latest Browse all 16408

CHID BENZI KUPANDISHWA KIZIMBANI KESHO KWA KUKAMATWA NA DAWA ZA KULEVYA

$
0
0
Ndugu wasomaji wetu tunaomba support yenu kwa kutangaza nasi hapa kwenye hii blog kwa bei nafuu ili tuweze kuendelea kutoa habari bila tatizo lolote. Wasiliana nasi kupitia namba +255713363965 / +255755274953. Tunashukuru kwa ushirikiano wenu. 

MSANII wa muziki wa hip hop, Rashid Makwiro ‘Chid Benzi’ anaendelea kushikiliwa na Jeshi la Polisi kwa tuhuma za kukamatwa na dawa za kulevya na kesho anatarajiwa kufikishwa mahakamani. 

Chidi Benzi alikamatwa na dawa za kulevya juzi jioni katika Uwanja wa Kimataifa Julius Nyerere, jijini Dar es Salaam wakatia wa ukaguzi kabla ya kupanda ndege ya Fastjet akielekea jijini Mbeya.

Kwa mujibu wa Kamanda wa Kuzuia na Kupambana na Madawa ya Kulevya Tanzania, SACP Alfred Nzowa, msanii huyo ameendelea kushikiliwa na jeshi la polisi mpaka kesho atakapofikishwa mahakamani.

Alisema Chidi Benz alikamatwa na dawa aina ya Heroine kete 14 na misokoto miwili ya bangi, vyote alikuwa ameiweka katika mfuko wa shati alilokuwa amevaa.

ENDELEA KUSOMA HABARI HII KWA KUBOFYA HAPA CHINI

“Dawa alizokamatwa nazo zilikuwa kwa ajili ya matumizi yake, jeshi limeendelea kumshikiria mpaka Jumatatu kwa sababu leo (jana) na kesho (leo) sio siku za kazi,” alisema.

Mbali ya dawa, msanii huyo alikutwa katika begi yake na kigae kidogo cha chungu na kijiko, ikiwa ni maandalizi ya kutumia dawa hizo.

Msanii huyo alikuwa anakwenda jijini Mbeya kwa shoo ya ‘Instagram Party’ iliyofanyika jana katika ukumbi wa City Pub, jijini humo.

Chidi Benzi alikuwa ameongozana na msanii mwenzake Nurdin Bilal ‘Shetta’ ambaye naye alishikiliwa kwa muda kabla ya kuachiliwa kuendelea na safari yake.

Viewing all articles
Browse latest Browse all 16408

Trending Articles



<script src="https://jsc.adskeeper.com/r/s/rssing.com.1596347.js" async> </script>